Swahili

KUTAFUTA IMANI LAKUNYOLOKA – AMA KI ORTHODOKSI (Σουαχίλι, Swahili)

25 Ιουλίου 2009

KUTAFUTA IMANI LAKUNYOLOKA – AMA KI ORTHODOKSI (Σουαχίλι, Swahili)

1)	Papa na Patriarki Aleksandria na wa Afrika mzima m.m.Theodoro wa pili anaonana na Mukantangezi-wa Kongo Mdocta Theologi pale Athina,Padiri Theotimu Tshal Mwin-kwa-Mpemb

1) Papa na Patriarki Aleksandria na wa Afrika mzima m.m.Theodoro wa pili anaonana na Mukantangezi-wa Kongo Mdocta Theologi pale Athina,Padiri Theotimu Tshal Mwin-kwa-Mpemb

Kutoka Padiri Mdocta Theologi Theotimu Kasomb Tshal Mwin-kwa-Mpemb.

Mambo la ufunulo la jangwa la Sahara juu ya Afrika ,vile  inakata mipaka kutosha Afrika la juu na Afrika chini la Sahara.Labda,Afrika juu la Sahara ina na waarabu waislamu, lakini Afrika chini la Sahara imebaki kwa wa afrikani weusi wa kweli,hizi mambo la ufunulo tunaitadji tu jifunze.

Fungulo la ufunulo hii ni NENO LA WOKOVU.

Kutoka wakati ule waarabu-islamu walifukuza wa afrikani weusi wenye mgini,awa walitelemuka mpaka chini la Sahara na kudjifungia katika kwabudu sanamu.Hata vile waafrikani weusi hawa kubaki kimia.Wamissionari kutoka Roma na dini la Romakatholika na wengine kutoka udongo la waengleza wenye dini lawa batizadji,walisafiri na kufika Uganda.Mambo njo,wamissionari wa ma dini hizi wakaanza kupigana nvita kwasababu dini tu moja ibaki.Labda,wamissionari wote wale walikuwa WAKRISTIANI.Matakizo ilikuwa kali sana mpaka waarabu-islamu nao walifika na kwanza nvita ingine.Ivi wa missionari wa liungana mu jina la Kristu wapate kufukuza ADUI WAO la dini la kiislamu.Wenye mgini,waafrikani weusi ama Baganda baada kuishi katika mapatikano hizi,hawa kupende tena kuchakuwa hata dini la wakristiani(Roma-katholika ama Babatizadji),hata kidogo dini la Islamu.

Moniale ama mwenyekudjitolea kwa Kristu (soeur) Thecla Namulej Mwin-kwa Mpemb. Alipataka kipawa la moniale mwaka 1988 na mkono ya Mweshimiwa Mkubwa Mzee Paoulo wa ku Rodo,lakini ku monasteri ya Bikira Maria pale Kalymnu.Sawa Mukatangezi-wa Kongo yeye ni Mwaafrika wa kwanza kupata hii kipawa.Anakaa Kolwezi na polelpole atakokota wabinti karibu naye.

Moniale ama mwenyekudjitolea kwa Kristu (soeur) Thecla Namulej Mwin-kwa Mpemb. Alipataka kipawa la moniale mwaka 1988 na mkono ya Mweshimiwa Mkubwa Mzee Paoulo wa ku Rodo,lakini ku monasteri ya Bikira Maria pale Kalymnu.Sawa Mukatangezi-wa Kongo yeye ni Mwaafrika wa kwanza kupata hii kipawa.Anakaa Kolwezi na polelpole atakokota wabinti karibu naye.

Baganda kutoka matatizo hizi,ilikuwa mwanzo la kutafuta IMANI LA KWELI njo Imani Lakunyoloka kutoka NENO LA WOKOVU.

Mwaka 1899,katika jamaa la wa limamashamba alizalikiwa muganda Sebanza Mukasa.Mwaka 1923 alibatiziwa mu dini la waengleza Kanisa Anglikan.Mpaka  mwaka 1928 alikuwa na tafuta dini la Kweli.Aliingia mu dini la wa Protestanti,alizungumuza nao lakini alitoka na akazungumuza na wenye dini la Romakatholika akaenda.Wakati alijifunza na wa missionari,adisi la wa Sparti askari miyunani ya zamani,alifurahiwa sana na akachakuwa jina mpya ama Sebanza Spartas.Mukwendeleya na kutafuta,akapata maandiko moja kama kuna mtu mojo ahitaji Marcus Garvey anakaa Karaϊbe na anatangaza Imani Lakunyoloka ama KI ORTHODOKSI.Mpembeni lake,ku Sud-Afrika kulikuwa vilevile wa tumishi wa Garvey.Mtafutadji la Ukweli Sebanza hakudjichungiye peke yake hii njia ya wokovu. Aliendaka  na akapasha habari kwa rafiki yake Basa-giakitalo uyu kumasiku kidogo aliwowa dada yake ya Sebanza na akakuwa semeki.Kutafuta kwa Sebanza ilikuwa tena kutafuta kwa Basa-giakitalo aliye zaliwa mwaka 1895.Watafutadji hawa wa wili hawakubaki tu wao  lakini walijulisha maitadji yao kwa rafiki wao mukenya Arthur Gaduna,naye akaitika akawafata wenzake.

Mumwaka 1930,mujumbe la watu moja wameitwa Orthodoksi walifika Uganda na Askofu wao Daniel-William Alexandre.Waitadji tatu wenye kutafuta Ukweli,walikaribisha wageni hawa na wakaitika mafundisho yao,wakabatiziwa na wa kapata sharimu ama wakawa mapadri.Baada ya masiku kidogo,yule Askofu aliondoka na kwende Sud-Afrika.Mapadri tatu hawa,wakaanza kufundisha dini mpya la Ki Orthodoksi katika Uganda na Kenya.Siku moja walipo fundisha Kampala,muyunani moja mu Orthodoksi wa kweli,akawachofeya na akawauliza hao ni wa nani?Wao wakadjibu.Sisi ni wapadri la dini  la ukweli ama ORTHODOKSI.

Mupadri Andre Kayaya amebatiza mumtoni kule Kananga

Mupadri Andre Kayaya amebatiza mumtoni kule Kananga

Muyunani yule akawa julisha kwamba:”Munadanganyiwa,ule Askofu Daniel ni mu OUNITI,nkundji moja ya Papa muroma-katholika inatangaza ki orthodoksi ya wongo.Hivi mwandike kwa padri muyunani orthodoksi wa kweli  jina lake NIKODEMU SARIKAS anakaa Moshi-Tanganika(1914-1919)”.Watafutadji tatu la IMANI LA KUNYOLOKA,waliandikaka bila kupitisha wakati,ivi ,Papa na mu Patriarki Aleksandria Meletio wa pili alitumaka miyumbe na mupadiri Nikodemu akawafikiya.Wakati walikusanika wote,wa padri tatu na waminifu wao wale waliitika kubatiziwa.Padri Nikodemu akasagaa sana na akasifu watafutadji tatu vile walifanya nguvu yote wafike ku kidjidji la IMANI LA UKWELI.

Mwanzo ya kutangaza Imani Lakunyoloka kule Uganda,watu wanakusanika ju wa fwate mafundisho.Banajenga kanisa ya udongo wapate namna ya kusala

Mwanzo ya kutangaza Imani Lakunyoloka kule Uganda,watu wanakusanika ju wa fwate mafundisho.Banajenga kanisa ya udongo wapate namna ya kusala

Mpadri muyunani Nikodemu akisha kujulisha Papa na Patriarki Aleksandria yakama watu hawa weko na hamu la Ki Orthodoksi lakini walidanganyiwa kwa wa ouniti-WAROMAKATHOLIKA.Mwisho,watafutadji tatu la Imani la Kunyoloka,walipata ruhusa,wakafundishwa na wa kapata Ukweli ule wa lianza kutafuta katika miaka kumi.Wakati wa libatiziwa na wa lipata kipawa la upadiri,majina lao ilikuwa :

Sebanza Mukasa Spartas Padri Rouvim,

Basagiakitalo                     Padri  Ovadia

Arthur  Gaduna                Padri  George.

Askofu mweusi wa kwanza,alikuwa mtafutadji la Imani Lakunyoloka,alipata kipawa la kipadiri na jina Rouvim mwaka 1933,mwisho akakuwa Askofu Nilopoli  Sebanza Mukasa Spartas Kristoforo (1899-1982).Alikuwa Muuganda

Askofu mweusi wa kwanza,alikuwa mtafutadji la Imani Lakunyoloka,alipata kipawa la kipadiri na jina Rouvim mwaka 1933,mwisho akakuwa Askofu Nilopoli Sebanza Mukasa Spartas Kristoforo (1899-1982).Alikuwa Muuganda

Mu Patriarki Aleksandria Meletio wa pili alifuraha sana na akaleta baraka kwa mwaafrika weusi watafutadji tatu la Imani la Kunyoloka waanze kupasha HABARI LA KI ORTHDOKSI mahali yeyote ya Afrika chini la Sahara.

Mupadri Mkubwa na Mzee Ovadia,alikuwa mtafutadji la Imani Lakunyoloka, Nkamboyake ya Askofu  Kampala Yona.Alitangaza Kiorthodoksi Uganda, Kenya mpaka  Tanzania.Baada alikuwa Mwenyeuganda(1895-1985)

Mupadri Mkubwa na Mzee Ovadia,alikuwa mtafutadji la Imani Lakunyoloka, Nkamboyake ya Askofu Kampala Yona.Alitangaza Kiorthodoksi Uganda, Kenya mpaka Tanzania.Baada alikuwa Mwenyeuganda(1895-1985)

Wakati lakutawala la Mu Patriarki Aleksandia Meletio wa pili(1926-1935),wapadiri awa wa tatu wa afrikani,walianza kutumika bila feza,bila saidizo yeyote,labda mpadri George Gaduna alirudi kwabo  ku Kenya na akaanza kutangaza NENO LA WOKOVU,namna moja na wa padiri Rouvim na Ovadia walianza kutangaza lile NENO fasi yote Uganda na Tanzania .Walijenga makanisa na masomo la nyasi.Ma elfu la binadamu walipokeya dini la UKWELI.

Mu Patriarki Aleksandria wasasa Nikolao wa tano(1935-1939),naye akisha kupata habari yakama Neno la Ki Orthodoksi inatangaziwa ku Afrika chini la Sahara ivi akaleta baraka ya maendeleyo.Muda kidogo,Patriarki wasasa Kristoforo(1939-1967),naye akashukuru vile Afrika chini la Sahara linapata Neno la Wokovu ili kutoka Aleksandria wao hawakuwezi miaki izi zote kutuma wapadiri wayunani ju ya wenye mgini.Ilikuwa magumu njo kwa sababu waarabu-islamu kule Afrika ya juu hawakupende wasikiye yakama, kutoka Misri,wa Orthodoksi wanatangaza dini lao kwa watu weusi.Habari la Imani  La Kunyoloka lili tangaziwa kwa nguvu la Roho Mtakatifu,katika mapendo la wenye mgini ivi baada ya miaka makumi mbili na mnane ,moyo wa Mu Patriarki Kristoforo ikapumzika na Patriarki wasasa akakuwa Nikolao wa sita(1967-1987).

Mu Patriarki Nikolao wa sita,akatazama ama miujiza la NENO LA WOKOVU katika Afrika chini la Sahara ivi akawaita wa tafutadji tatu la Imani La Kunyoloka kule Aleksandria akawapigia aksante,akawaombea na akaleta vipawa vya juu kwa padiri Rouvim Spartas Sebanza akakuwa Askofu mweusi wakwanza na jina la sasa KRISTOFORO Askofu wa Mudji la Mtoni Mkubwa Nilo ama Nilopoli,baada mu padiri George Gaduna akakuwa Askofu mweusi wa pili na jina Nitria.Padri Ovadia Basagiakitalo akabaki Mzee wa wapadiri kwa sababubu aliishi na jama lake.Hii mambo lakutafuta Imani Lakunyoloka ama Kiorthodoksi,ilikuwa Neno la Ufunulo kwa watu weusi.Wakati Askofu wakwanza mweusi  Kristoforo alipata hii kipawa,naye akachaguwa vyjana waende Aleksandria na ku mudji la wayunani wapate kujifunza na warudi wendeleshe kazi la shamba la Bwana.Kijana wa kwanza akaisha kujifunza akarudi na akawa Mudiako,kiisha Mupadiri na mwisho akawa Askofu mweusi wa tatu Theodoro Nakyama Askofu Kampala na Uganda mzima wakati wa Mu Patriarki Parthenio wa tatu(1987-1996).Kiisha,wakati wa Patriarki Petro wa saba (1997-2004),alitwaa kipawa ya Askofu mweusi wa ine kwa Mtheologi na Mufilosofu Yona Lwanga,uyu ni mtoto wa mtoto wa Mzee Padiri Ovadia Basagiakitalo.

Askofu wa Kampala na Uganda mzima m. Yona Lwanga(1992)ni Askofu wa ine alikuwa Muuganda

Askofu wa Kampala na Uganda mzima m. Yona Lwanga(1992)ni Askofu wa ine alikuwa Muuganda

Ilikuwa furaha sana ,hata  nkambo hakupata kipawa ya Askofu,lakini munkana anapata ile baraka akakuwa Askofu mweusi wa ine(1992) mbele Msaidizi-Bukoba,kiisha, pa fasi ya Kampala na Uganda mzima mwaka 1997.Maendeleo haya ya baganda ina mpaka  mwaka 1999,Askofu wa tano mweusi akapata kipawa kwanza sawa Msaidizi Bukoba.Sasa kutoka pale anakuwa Patriarki Theodoro wa pili(2004) na yeye akamfanya Muuganda Askofu mweusi  wa tano  Yeronimo Mzee akawa Askofu Mwanza-Tanzania 2009,alafu alikuwa Msaidizi toka miaka kumi.Hizi ndivyo NENO LA UFUNULO katika mambo la KUTAFUTA IMANI LAKUYNOLOKA AMA KIORTHODOKSI.Wenye kusikiya hamu la kupata UKWELI, fungulo la kidjidji ama chemuchemu ni NENO LA WOKOVU,lina tosha watu mungiza na mu madini la sanamu ju ya kuwapeleka kwenye Mwangaza inatoka wapate Roho Mtakatifu Mkamilifu katika Bwana Yesu Kristu Mwokovu wetu na Mpenda wanadamu kwa mapendo ya Baba Mwenyezi Mtatu Mtakatifu.

Watafutadji la Imani La Kweli walianza kujenga makanisa ya udongo na mamasomo kwa sababu hawa kukuwe na saidizo

Watafutadji la Imani La Kweli walianza kujenga makanisa ya udongo na mamasomo kwa sababu hawa kukuwe na saidizo